Logo video2dn
  • Сохранить видео с ютуба
  • Категории
    • Музыка
    • Кино и Анимация
    • Автомобили
    • Животные
    • Спорт
    • Путешествия
    • Игры
    • Люди и Блоги
    • Юмор
    • Развлечения
    • Новости и Политика
    • Howto и Стиль
    • Diy своими руками
    • Образование
    • Наука и Технологии
    • Некоммерческие Организации
  • О сайте

Скачать или смотреть UKWELI WOTE SABABU ZA VIJANA 170 KULUNA KUUAWA CONGO DR

  • Mwananchi Digital
  • 2025-01-14
  • 288931
UKWELI WOTE SABABU ZA  VIJANA 170 KULUNA KUUAWA  CONGO DR
  • ok logo

Скачать UKWELI WOTE SABABU ZA VIJANA 170 KULUNA KUUAWA CONGO DR бесплатно в качестве 4к (2к / 1080p)

У нас вы можете скачать бесплатно UKWELI WOTE SABABU ZA VIJANA 170 KULUNA KUUAWA CONGO DR или посмотреть видео с ютуба в максимальном доступном качестве.

Для скачивания выберите вариант из формы ниже:

  • Информация по загрузке:

Cкачать музыку UKWELI WOTE SABABU ZA VIJANA 170 KULUNA KUUAWA CONGO DR бесплатно в формате MP3:

Если иконки загрузки не отобразились, ПОЖАЛУЙСТА, НАЖМИТЕ ЗДЕСЬ или обновите страницу
Если у вас возникли трудности с загрузкой, пожалуйста, свяжитесь с нами по контактам, указанным в нижней части страницы.
Спасибо за использование сервиса video2dn.com

Описание к видео UKWELI WOTE SABABU ZA VIJANA 170 KULUNA KUUAWA CONGO DR

Kinshasa. Serikali nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo inadaiwa kuwaua vijana 170 waliokamatwa kwa madai ya kuwa wanachama wa makundi yanayotekeleza uhalifu wa mjini maarufu kama “Kuluna.”

Vyombo vya Habari vya ndani Congo vinawaonyesha vijana hao wakiwa wamefungwa pingu mikononi huku wakibubujikwa machozi wakati wakisikiliza hotuba ya Waziri wa Sheria wa taifa hilo, Constant Mutamba.

Shirika la Kimataifa la Kutetea Haki za Binadamu la Amnesty International limeripoti kuwa mamlaka za usalama nchini humo zimewakamata watuhumiwa zaidi ya 1,400 wa uhalifu huku wakitajwa kuwa ni wanachama wa Kundi la Kuluna.

Amnesty International pia imesema kuwa kati ya waliokamatwa wengi wao ni vijana wenye umri kati ya miaka 18 hadi 35 ambao wanadaiwa kutenda makosa ya uhalifu ikiwemo uvamizi wa makazi na mauaji ya raia.

Shirika la Habari la Associated Press limeripoti kuwa vijana takriban 170 kati yao wameshahukumiwa adhabu ya kifo na tayari taarifa zinadai kuwa vijana hao wameshauawa kwa kupigwa risasi nchini humo.

Vijana hao walikamatwa kupitia Opereshezi za usalama zilizofanyika eneo la Ndobo, Lingala kwa lengo la kuwakamata vijana hao kati ya Desemba zikiongozwa waziri, Mutamba zililenga kukomesha magenge ya wahalifu katika Mji wa Ndobo wenye wakazi zaidi ya milioni 15.

Shirika la Habari Associated Press limeripoti kuwa vijana hao walihamishwa kwa makundi makundi kutoka katika Gereza lililoko Jijini Kinshasa kwenda katika gereza lililoko mafichoni na lenye ulinzi wa hali ya juu kwa ajili ya kwenda kuuawa.

Kwa mujibu wa Waziri wa Sheria nchini Congo, Mutamba, wafungwa 70 kati yao walisafirishwa siku ya Jumapili huku wengine 102 wakipelekwa katika gereza la Angenga lililopo Kaskazini mwa Jimbo la Mongala nchini humo.

Mutamba alisema vijana wote wa Kuluna walikutwa na hatia ya kufanya uhalifu wa mijini ‘urban bandits’ na wana umri kati ya miaka 18 hadi 35, japo hakuweka wazi ni lini vijana hao watauawa.

Baadhi ya raia wa Congo DR wamepongeza uamuzi huo kwa kile wanachosema itasaidia kupunguza hofu iliyoibuliwa na matukio ya vijana hao huku wengine wakihofia kuwa kutekelezwa kwa adhabu ya kifo dhidi ya vijana hao kuwa ni ukatili na uvunjaji wa haki za binadamu.

“Tunakubaliana na uamuzi huu wa waziri wa Sheria kwa sababu unalenga kukomesha uhalifu maeneo ya mjini. Awali ilikuwa ikifika Saa 2:00 usiku tu hauwezi tena kutembea mtaani ukiwa huru kwa sababu ya kuhofia vijana wa kundi la Kuluna,” Mkazi wa Goma Mashariki, Fiston Kakule, aliieleza Associated Press.

Espoir Muhinuka, ambaye ni Mwanaharakati wa Haki za Binadamu alionya kuwa kuuawa kwa vijana hao huenda kukakiuka msingi wa utoaji wa haki na kuzitaka mamlaka nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo kuheshimu haki za binadamu.

Mwanaharakati huyo alisem anahofia kuwa huenda msukumo wa kisiasa ukasababisha uvunjaji wa haki na kusababisha watu kushtakiwa kisha kuuawa bila kufuata mfumo halali wa utoaji haki nchini humo.

“Hali inayoendelea nchini Congo DR inachanganya na inahitaji Jumuiya ya Kimataifa kuingilia kati. Mapambano dhidi ya makundi ya uhalifu ya Mjini yanapaswa kwenda sawia na kuondoa Umaskini, ukosefu wa ajira na utengano wa jamii ambao wote unachangia kuibuka kwa makundi haya,” alisema mwanaharakati huyo.

Congo ilifuta hukumu ya kifo mwaka 1981, kisha kuirejesha mwaka 2006. Mauaji ya mwisho kutokana na hukumu hiyo yalitekelezwa mwaka 2003.

Machi 2024, Serikali ya Congo, ilitangaza utekelezwaji wa adhabu hiyo kwa watu wlaiotiwa hatiani kwa makosa makubwa ya uhalifu ikiwemo Uhaini.

Mwezi Mei 2024, wanajeshi nane wa Jeshi la Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo walitiwa hatiani na kuhukumiwa adhabu ya kifo na Julai 2024, wanajedhi wengine 25 nao walitiwa hatiani kwa kosa la aina hiyo japo wote hawafahamiki waliko hadi sasa na haifahamiki iwapo wameshauawa ama la.

Kutokana na kisa cha kuhukumiwa adhabu ya kifo kwa vijana hao, Naibu Mkurugenzi wa Shirika la Amnesty International Mashariki na Kusini mwa Afrika, Sarah Jackson, alisema:

“Taarifa ya kuhamishwa kwa wafungwa hao kunashtua sana. Tunahofia kuwa kutasababisha mauaji ya wafungwa kwa wingi yanayotekelezwa na Serikali kutokana na kwamba hakuna uwazi wakati wa utekelezaji wa adhabu na hatujui wangapi wameshauawa na ni kina nani,”

“Rais Felix Tshisekedi anatakiwa asitishe mara moja na kutangaza kwa Umma kusitishwa kwa mauaji ya wafungwa katika gereza la Angenga na maeneo mengine. Bunge linapaswa kuja na mswada wa dharura kuzuia mauaji ya vijana hao na kuiondoa kabisa adhabu ya kifo,” aliandika Sara.

“Mamlaka pia zinapaswa kuacha tabia ya kuwahamisha wafungwa kuwapeleka katika magereza yenye ulinzi mkali vijijini ikiwemo gereza la Angenga ambako idadi kubwa ya wafungwa wamepelekwa kufariki kwa kuuawa, njaa ama magonjwa,”

“Kila mfungwa anayefungwa katika eneo lake anapaswa kufungwa katika gereza ambalo linaweza kufikiwa na mwanasheria, ndugu, na taasisi za Haki za Binadamu kwa urahisi, na wanapaswa kufahamika walipo,” aliandika.

Комментарии

Информация по комментариям в разработке

Похожие видео

  • RDC : Retour sur  le Kuluna qui a coupé la Main sans pitié, Mutamba très Choqué, Peine de mort tombe
    RDC : Retour sur le Kuluna qui a coupé la Main sans pitié, Mutamba très Choqué, Peine de mort tombe
    1 год назад
  • Киллер Путина. О чем пять лет молчал убийца из Берлина | Черное дело
    Киллер Путина. О чем пять лет молчал убийца из Берлина | Черное дело
    8 часов назад
  • Kaya 14 zakosa makazi Moshi baada ya nyumba zao kuzingirwa na mafuriko
    Kaya 14 zakosa makazi Moshi baada ya nyumba zao kuzingirwa na mafuriko
    1 день назад
  • BBC SWAHILI HALI INAZIDI KUWA TETE MASHARIKI YA KATI
    BBC SWAHILI HALI INAZIDI KUWA TETE MASHARIKI YA KATI
    1 день назад
  • 🛑DIRECT ANGENGA EXÉCUTION P€INE DE M0RT MUTAMBA TRÈS F€RME, DÉPART S/TENSI0N DES KULUNA C0NDAMN€S
    🛑DIRECT ANGENGA EXÉCUTION P€INE DE M0RT MUTAMBA TRÈS F€RME, DÉPART S/TENSI0N DES KULUNA C0NDAMN€S
    1 год назад
  • ⚡️НОВОСТИ | ЭВАКУАЦИЯ | БИРЖЕВОЙ ОБВАЛ | РОССИЯНЕ ХОТЯТ ЗАКОНЧИТЬ ВОЙНУ | ТАЙНАЯ СДЕЛКА РОССИИ
    ⚡️НОВОСТИ | ЭВАКУАЦИЯ | БИРЖЕВОЙ ОБВАЛ | РОССИЯНЕ ХОТЯТ ЗАКОНЧИТЬ ВОЙНУ | ТАЙНАЯ СДЕЛКА РОССИИ
    4 часа назад
  • «Начались чистки». Соловьев выгоняет ведущих за критику мессенджера Макс
    «Начались чистки». Соловьев выгоняет ведущих за критику мессенджера Макс
    3 часа назад
  • NEMC YABAINI KIWANDA BUBU KINACHOZALISHA MIFUKO YA PLASTIKI KINYUME NA SHERIA YA MAZINGIRA
    NEMC YABAINI KIWANDA BUBU KINACHOZALISHA MIFUKO YA PLASTIKI KINYUME NA SHERIA YA MAZINGIRA
    3 года назад
  • 🚨KISUGU,ACHAFUKWA AMJIBU ALIKAMWE,AIBUKIA KOCHA YANGA KUTIMULIWA.
    🚨KISUGU,ACHAFUKWA AMJIBU ALIKAMWE,AIBUKIA KOCHA YANGA KUTIMULIWA.
    5 часов назад
  • ⚡️НОВОСТИ | СБИТ РОССИЙСКИЙ ВЕРТОЛЕТ | ЗАПРЕТ НА ВЫЕЗД УЖЕ РАБОТАЕТ | ТРАМП НАЧАЛ ЕЩЕ ОДНУ «СВО»
    ⚡️НОВОСТИ | СБИТ РОССИЙСКИЙ ВЕРТОЛЕТ | ЗАПРЕТ НА ВЫЕЗД УЖЕ РАБОТАЕТ | ТРАМП НАЧАЛ ЕЩЕ ОДНУ «СВО»
    10 часов назад
  • ‼️Иран ударил по Турции. Атакованы ядерные объекты и флот Ирана. Операция в Ливане / Выпуск новостей
    ‼️Иран ударил по Турции. Атакованы ядерные объекты и флот Ирана. Операция в Ливане / Выпуск новостей
    Трансляция закончилась 58 минут назад
  • #EXCLUSIVE AMBOKILE AMCHANA AHMED ALLY BAADA YA KUMUITA CHAWA WA GSM,UKWELI UNAWAUMA WANASIMBA SANA!
    #EXCLUSIVE AMBOKILE AMCHANA AHMED ALLY BAADA YA KUMUITA CHAWA WA GSM,UKWELI UNAWAUMA WANASIMBA SANA!
    2 часа назад
  • 🤯Кремль ПЕРЕВЕРНУЛ ВСЁ ЭТИМ ответом Ирану! Вот, что ЗАДУМАЛ Трамп. Путин ТРЯСЕТСЯ ЗА ШКУРУ. ГУДКОВ
    🤯Кремль ПЕРЕВЕРНУЛ ВСЁ ЭТИМ ответом Ирану! Вот, что ЗАДУМАЛ Трамп. Путин ТРЯСЕТСЯ ЗА ШКУРУ. ГУДКОВ
    4 часа назад
  • Choc à Kinshasa: Plus de 100 Kuluna neutralisés au Camp Luka ! Opération coup de poing de la police
    Choc à Kinshasa: Plus de 100 Kuluna neutralisés au Camp Luka ! Opération coup de poing de la police
    1 год назад
  • Авиаудар в самое сердце Ирана / Верхушка режима ликвидирована?
    Авиаудар в самое сердце Ирана / Верхушка режима ликвидирована?
    14 часов назад
  • Точечный удар: как нашли секретный штаб Израиля - Скотт Риттер
    Точечный удар: как нашли секретный штаб Израиля - Скотт Риттер
    2 часа назад
  • Массированные бомбардировки Ирана. Крупнейшая воздушная операция Израиля и США
    Массированные бомбардировки Ирана. Крупнейшая воздушная операция Израиля и США
    8 часов назад
  • DJ SMA : afichua siri KUHUSU IRAN kusaidiwa na PUTIN/ MAREKANI na ISRAEL wajipange VITA BADO IPO
    DJ SMA : afichua siri KUHUSU IRAN kusaidiwa na PUTIN/ MAREKANI na ISRAEL wajipange VITA BADO IPO
    22 часа назад
  • ГЕВОРГЯН: Трамп готов на ЛЮБЫЕ ЖЕРТВЫ! // Война на Ближнем Востоке НЕ ЗАКОНЧИТСЯ?
    ГЕВОРГЯН: Трамп готов на ЛЮБЫЕ ЖЕРТВЫ! // Война на Ближнем Востоке НЕ ЗАКОНЧИТСЯ?
    8 часов назад
  • Как выследили Аятоллу и как выследят Путина | Диктатуры и технологии (English subtitles) @Max_Katz
    Как выследили Аятоллу и как выследят Путина | Диктатуры и технологии (English subtitles) @Max_Katz
    7 часов назад
  • О нас
  • Контакты
  • Отказ от ответственности - Disclaimer
  • Условия использования сайта - TOS
  • Политика конфиденциальности

video2dn Copyright © 2023 - 2025

Контакты для правообладателей video2contact@gmail.com