Pr. Dr .Blasious Ruguri ;Tatizo kubwa ni kutofahamu kuwa una mamlaka.

Описание к видео Pr. Dr .Blasious Ruguri ;Tatizo kubwa ni kutofahamu kuwa una mamlaka.

Mwenyekiti wa Kanda ya Afrika Mashariki na kati wa kanisa la waadventista wasabato,Daktari Blasious Ruguri awaasa wachungaji kuwa na Imani kubwa kwa Mungu kwani amewapa mamlaka ya kufanya hivyo kama watumishi wake au wawakilishi wake duniani.
Ameyasema hayo akiwa katika mkutano wa mwishoni mwa mwaka katika ofisi za jimbo kuu la Kaskazini mwa Tanzania la Waadventista wasabato jijini Arusha ambapo atakuwa na siku mbili za kuzungumza na viongozi wa Jimbo hilo la kaskazini, Ambao ni pamoja na maofisa watatu wa jimbo hilo Daktari Godwin Lekundayo(Mwenyekiti),Mchungaji Daudi Makoye(Katibu) ,Bwana Dickson Matiko(Muhazini)
Aidha mkutano huo umejumuisha maofisa watatu wa kila jimbo dogo linalounda Jimbo kuu hilo,wakurugenzi wote wa idara katika ofisi kuu za jimbo pamoja na viongozi wa taasisi mbalimbali za kanisa zilizopo jimboni humo.
Lengo la mkutano huo unaofanyika kila mwaka ni kutathmini utendaji kazi kupitisha bajeti kwa ajili ya matumizi ya mwaka unaofuata 2018.

Комментарии

Информация по комментариям в разработке