Sugu aanza mikutano, amtaka Dk Tulia wakutane 2025 jimboni

Описание к видео Sugu aanza mikutano, amtaka Dk Tulia wakutane 2025 jimboni

"Tunakutaka Tulia, tunakutaka Tulia tunakutaka Tulia" ni kauli ya mbunge wa zamani wa Mbeya Mjini wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Joseph Mbilinyi 'Sugu' akielezea hoja ya ugawaji wa Jimbo la Mbeya mjini iliyowasilishwa bungeni hivi karibuni.

Sugu ambaye aliwahi kuwa mbunge wa Jimbo hilo kwa kipindi cha miaka 10, (2010 Hadi 2020) kabla ya uchaguzi Mkuu uliopita kuchukuliwa na Dr Tulia Ackson ambaye pia ni spika wa bunge kwa sasa.

Akizungumza leo Alhamisi Mei 11, 2023 kwenye mkutano wake wa hadhara uliofanyika katika Kata ya Nzovwe jijini hapa, Sugu amesema alisikia hoja hiyo lakini hakuwahi kulielezea popote akisisitiza kuwa yeye analitaka Jimbo la Mbeya mjini.

Amesema yeye akiwa mbunge aliweza kuzihudumia Kata zote 36 za Jimbo hilo, lakini anashangaa hoja ya kuligawa na kwamba vyovyote iwavyo anamtaka Dk Tulia Ackson popote.

"Nashangaa kwanini huyu spika anapaniki tu, mimi sijaongea chochote tayari ameanza kuzungumzia hili jambo, sasa nasema hivi tukutane 2025 kwani aliyemuweka bungeni kwa sasa hayupo tena,"

Комментарии

Информация по комментариям в разработке