Salama Na ROSE MUHANDO SE6 EP53 | NIPE UVUMILIVU PART 2 | SendTip MPESA LIPA NO 5578460

Описание к видео Salama Na ROSE MUHANDO SE6 EP53 | NIPE UVUMILIVU PART 2 | SendTip MPESA LIPA NO 5578460

#SalamaNa #SendTip Through MPESA #5578460

Katika binadamu ambao walinipa wakati mgumu na kusubiri kwingi kabla ya kuja kukaa kwenye meza yetu ya kigae na kiti chakavu basi mmoja wao ni Rose huyu wa Muhando. Upatikanaji wake ni kama ukitaka kumuona SIMBA mbugani, lazima uamke asubuhi na mapema au uwe na bahati ya mtende kama ambayo sisi tumepata. Ingawa tulisubiri kwa masiku tele na miezi tele katikati ya mwaka huu tuliweza kumpata na kukaa nae chini ili tuweze kuzungumza nae.
Rose ni wa moto sana, kalenda yake imejaa safari tele za nje na ndani ya nchi, anazunguka mara kwa mara kwaajili ya kutoa elimu na burudani kwa watu wengi ambao nao pia wamekua wakimgojea kwa hamu na kwa masiku tele. Kipaji chake cha kipekee ndicho ambacho kimemfanya awe maalum miungoni mwa wasanii wanaofanya muziki wa Injili na uzuri wake mwengine ni kwamba amekua akitoa huduma hiyo kwa miaka mingi bila ya ‘kuchuja’.
Sasa nini hasa siri ya mafanikio hayo?! Ukiachana na panda shuka tele ambazo Rose amepitia toka akiwa na umri wa miaka 6, kukata tamaa ni jambo ambalo halipo kabisa katika mambo ambayo huwa anayawaza. Pengine kujiuliza kwanini na anatokaje kwenye hilo zito alilo nalo linaweza likawa ndo swali, ila kusema kwamba hatoweza au haiwezekani hilo jambo kwenye kitabu chake au kichwani chake huwa halipo kabisa.
Ukiskiliza kwa makini maneno ambayo yanatoka katika mdomo wake utagundua Rose ni mmoja kati ya wanawake jasiri sana ambao wamewahi kutokea katika kiwanda hiki cha Sanaa hapa Tanzania. Ukimuangalia macho yake, mikono yake ambayo imejaa makovu na nna uhakika pia kuna sehemu nyengine kwenye mwili wake pia zimejaa makovu lakini hatukuweza kuona unaweza ukapata tu idea ya makubwa na mazito ambayo amepitia na ambayo yameacha makovu makubwa tu si mwilini mwake tu bali hata kwenye moyo wake. Ananihadithia kwenye episode hii jinsi ambavyo watu walikua wanamuadhibu ki mwili na ki akili ikiwa ni pamoja na kupigwa, kuchomwa moto, kukatwa na kunyang’anywa mali zote ambazo amewahi kutengeneza tokea wakati anaanza muziki ila hayo yote hayajawahi kumkatisha tamaa wala kumrudisha nyuma.
Rose anaamini na aliamini kwamba ana uwezo wa kuvipata vyote ambavyo watu walimdhulumu kwenye kipindi flani kwenye maisha yake, aliamini hakuna ambaye anaweza kumnyang’anya kipaji ambacho Mwenyezi Mungu amempatia na kwa kupitia hiko kipaji na akiwa hai na mzima basi vyote ambavyo aliwahi kuwa navyo na vikapotea basi alikua na uwezo wa kuvirudisha na ni kweli, kuvirudisha ameweza na vimekuja maradufu yake.
Simulizi zake za safari yake toka siku ya kwanza alipokua mdogo nyumbani kwa Baba na Mama yake huko kwao Morogoro wakati anaumwa ni moja ya vitu vya kufikirisha sana ambavyo nimewahi kuvisikia toka tumeanza kukalia kiti chakavu, na yangu matumaini maongezi haya kwa kiasi kikubwa yatakupa ile vibe ambayo huwa naizungumzia kwenye intro ya kipindi chetu hiki.
Tafadhali enjoy.
Love,
Salama.

Support us through https://anchor.fm/yahstonetown/support
SUBSRIBE TO OUR CHANNEL https://bit.ly/YahStoneTownSubs

Listen our Podcast on
Spotify Link https://spoti.fi/2Uxr6Cm‬
‪ApplePodcast Link https://apple.co/2Ou1bru‬
GooglePodcast Link https://bit.ly/GooglePodcastSalamaNa
Audiomack Link https://bit.ly/YahStoneTownAudioMack
‪YouTube Link http://bit.ly/YoutubeSalamaNa

Soundtrack Yeah by @MarcoChali    • Marco Chali Feat One The Incredible &...  

Follow:
Twitter:   / yahstonetown  
Instagram:   / yahstonetown  
Facebook:   / yahstonetown  

Channel Administered by Slide Digital
Instagram: www.instagram.com/slidedigitaltz

Комментарии

Информация по комментариям в разработке