UPIGAJI WIZARA YA FEDHA, WAZIRI MKUU AWASIMAMISHA KAZI VIGOGO, ATOA MAELEKEZO KWA KAMISHNA TAKUKURU

Описание к видео UPIGAJI WIZARA YA FEDHA, WAZIRI MKUU AWASIMAMISHA KAZI VIGOGO, ATOA MAELEKEZO KWA KAMISHNA TAKUKURU

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa amewasimamisha kazi Mkaguzi Mkuu, Mkaguzi Msaidizi pamoja na baadhi ya watendaji wa Wizara ya Fedha na Mipango ili kupisha uchunguzi wa tuhuma za matumizi mabaya ya fedha za umma zinazowakabili.

Akizungumza katika Kikao Kazi na Waziri wa Fedha na Mipango, Kaibu Mkuu, Manaibu Katibu Wakuu na Watendaji Waandamizi wa Wizara hiyo kwenye ukumbi wa Hazina jijini Dodoma Mei 27, 2021, Majaliwa amemuagiza Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Kamishna wa Polisi CP Salum Rashid Hamdun kufanya uchunguzi kuhusu tuhuma hizo na ikithibitika kwamba tuhuma si za kweli wahusika watarejeshwa kazini..
#MillardAyoUPDATES

Комментарии

Информация по комментариям в разработке