Salama Na DULLA Ep 39 | GO HARD OR GO HOME... Part 1

Описание к видео Salama Na DULLA Ep 39 | GO HARD OR GO HOME... Part 1

#SalamaNa #SendTip #0762797291
You Can support US through https://anchor.fm/yahstonetown/support
SUBSRIBE TO OUR CHANNEL https://bit.ly/YahStoneTownSubs

Listen our Podcast on
Spotify Link https://spoti.fi/2Uxr6Cm‬
‪ApplePodcast Link https://apple.co/2Ou1bru‬
GooglePodcast Link https://bit.ly/GooglePodcastSalamaNa
Audiomack Link https://bit.ly/YahStoneTownAudioMack
‪YouTube Link http://bit.ly/YoutubeSalamaNa

Abdallah Khamis Ambua ndo jina halisi toka kwa wazazi wake ambao hawana asili ya kisiwani wala kuwahi kuishi huko kwa muda mrefu ambako pengine ndo kukamuwezesha kupata hiyo lafdhi. Kabla hatujafika kokote kwa kuskia kutoka kwangu, ningepeda ufahamu kwamba mimi si mmoja ya watu walotaka Dulla apewe kipindi cha Planet Bongo mwaka 2018 wakati naenda zangu Cardiff kushangaa kondoo, na moja ya sababu zangu kubwa ilikua yeye kutokua na lafdhi nzuri ya maneno kwenye lugha yetu adhimu ya Kiswahili. Na hilo nililiweka wazi haswa. Lakini pia nilikubaliana na matokeo baada ya viongozi kuamua kumpitisha yeye, na kwa heshima zote leo napenda kuchukua nafasi hii kuwapongeza kwa kazi nzuri waliyoifanya, kwa kuona kijana ambaye alikua na utayari kwa kujifunza, wa kujua kwamba alikua hajakamilika na mlango ukawa wazi kwake kutaka kujifunza na kuwa bora.

Tupeleke miaka mbele mpaka 2020, ingawa hapo nyuma tushakutana mara kadhaa na nikamuambia jinsi ambavyo ananifurahisha kwa kukuwa kwake na kwamba mimi ni mmoja wa watu wanao jivunia yeye. Na hata wakati tunafanya maongezi yetu haya, nilimfahamisha pia. Mwanzo wakati naanza kuandika nilianza kwa kukuambia kuhusu asili yake, sababu ilikua ni juu ya lafdhi yake ya kimwambao ilonyooka haswa. Mimi wakati nakutana na Dulla kwa mara ya kwanza kwenye usaili hakua na hiyo accent, alikua na matatizo ya R na L na pia hakua ‘original’, alikua ana tangaza na kuongea kama B Dozen, ambaye tayari alikua amesha ji establish vizuri tu na anga yote alikua anaunguruma yeye mara ifikapo saa nane kamili ya mchana. So kama mtangazaji mpya anayechipukia, Dulla hakua na nafasi ya kuweza kutamba mbele ya Dozen, na wala hakua na uwezo wa hata robo yake. Kwa yeye kutoboa na kuweka alama yake ilikua inambidi awe YEYE na aje na ladha YAKE.

Leo hii, mimi na enjoy haswa ninapomsikiliza Mjukuu wa Ambua radioni, sauti tamu, matamshi yamenyooka, ladha ya maneno inatulia maskioni, hapayukwi kwenye kipaza sauti na pia kubwa kuliko yote ana akili, akili ya kusema na kuuliza maswali muafaka na muda muafaka. Na kwa hilo namheshimu.

Basi nikataka kujua vile alijiskia alipong’amua kama mimi sikua shabiki yake hata kidogo? Na Kama ilimtoa katika ‘mchezo?’. Wakati mshindi wa mtangazaji mpya wa Planet Bongo anatangazwa tayari Mimi nilikua nishafika zangu Cardiff kwahiyo sikuwahi kuongea nae tena kuhusu uchaguzi wake na wala maendeleo yake kwahiyo hii imekua mara ya kwanza tuna discuss. Pia nilitaka kujua kuhusu mke wake, watoto, Kaka yake ambaye naye ndo alimfanya kwa kiasi kikubwa achague kazi hii anayofanya sasa. Pia kuhusu mahusiano yake na Diamond Platnumz na Ali Kiba, muziki wa Bongo Flava kwa ujumla. Kazi, mapenzi, ujana, dini na yeye kama binadamu. Haya yalikua maongezi flani ya kikubwa ambayo nimefurahi tuliyafanya mimi na mdogo wangu huyu.

Kama kawaida, yangu matumaini hii pia itakufunza jambo, itakutaka uwe bora na kutokubali kushidwa hata kama ulokua unapenda sana akupe sapoti akawa haamini juu ya uwezo wako, hiyo ndo iwe chachu ya wewe kutaka kufanya vyema zaidi.

Love,
Salama


Soundtrack Yeah by @MarcoChali    • Marco Chali Feat One The Incredible &...  

Follow:
Twitter:   / yahstonetown  
Instagram:   / yahstonetown  
Facebook:   / yahstonetown  

Комментарии

Информация по комментариям в разработке