KIJITONYAMA LUTHERAN CHURCH : IBADA YA JUMAPILI 09 NOVEMBER 2025
UJUMBE WA LEO: "TUVUMILIE HATA MWISHO KATIKA BWANA"
Mathayo 24:1 - 13
1 Yesu akaenda zake, akatoka hekaluni; wanafunzi wake wakamwendea ili kumwonyesha majengo ya hekalu.
2 Naye akajibu akawaambia, Hamyaoni haya yote? Amin, nawaambieni, Halitasalia hapa jiwe juu ya jiwe ambalo halitabomoshwa.
3 Hata alipokuwa ameketi katika mlima wa Mizeituni, wanafunzi wake wakamwendea kwa faragha, wakisema, Tuambie, mambo hayo yatakuwa lini? Nayo ni nini dalili ya kuja kwako, na ya mwisho wa dunia?
4 Yesu akajibu, akawaambia, Angalieni, mtu asiwadanganye.
5 Kwa sababu wengi watakuja kwa jina langu, wakisema, Mimi ni Kristo; nao watadanganya wengi.
6 Nanyi mtasikia habari za vita na matetesi ya vita; angalieni, msitishwe; maana hayo hayana budi kutukia; lakini ule mwisho bado.
7 Kwa maana taifa litaondoka kupigana na taifa, na ufalme kupigana na ufalme; kutakuwa na njaa, na matetemeko ya nchi mahali mahali.
8 Hayo yote ndiyo mwanzo wa utungu.
9 Wakati huo watawasaliti ninyi mpate dhiki, nao watawaua; nanyi mtakuwa watu wa kuchukiwa na mataifa yote kwa ajili ya jina langu.
10 Ndipo wengi watakapojikwaa, nao watasalitiana, na kuchukiana.
11 Na manabii wengi wa uongo watatokea, na kudanganya wengi.
12 Na kwa sababu ya kuongezeka maasi, upendo wa wengi utapoa.
13 Lakini mwenye kuvumilia hata mwisho, ndiye atakayeokoka.
1. KUVUMILIA DHIKI NA UTUNGU WA MWISHO WA DUNIA ULIOJAA
MAJANGA NA HATARI...
KWA KUWA UPENDO WA WENGI UTAPOA NA
KUTAKUWA NA USALITI NA CHUKI...
SAWA NA NENO LA NABII
Isaya 24 : 16 - 20
16 Toka pande za mwisho wa dunia tumesikia nyimbo, Atukuzwe mwenye haki. Ndipo niliposema, Kukonda kwangu! Kukonda kwangu! Ole wangu! Watenda hila wametenda hila, naam, watendao hila wametenda hila sana.
17 Hofu, na shimo, na mtego, vi juu yako, Ee mwenye kukaa duniani.
18 Itakuwa kila akimbiaye sauti ya hofu ataanguka katika shimo; na kila apandaye na kutoka shimoni atanaswa na mtego; kwa maana madirisha yaliyo juu yamewekwa wazi, na misingi ya dunia inatikisika.
19 Dunia kuvunjika, inavunjika sana; dunia kupasuka, imepasuka sana; dunia kutikisika, imetikisika sana.
20 Dunia inalewa-lewa kama mlevi, nayo inawaya-waya kama machela; na mzigo wa dhambi zake utailemea; nayo itaanguka, wala haitainuka tena.
2. MATETEMEKO YA NCHI MAHALI MAHALI DUNIANI KOTE...
Mathayo 24 : 7
7 Kwa maana taifa litaondoka kupigana na taifa, na ufalme kupigana na ufalme; kutakuwa na njaa, na matetemeko ya nchi mahali mahali.
3. MAJANGA HAYA YA DUNIA HUWA YANALETA TRAUMA NDANI YA WATU.
"MAANA YA “TRAUMA”
Neno trauma linamaanisha mshtuko mkubwa wa kihisia au kimwili unaotokea
baada ya mtu kupitia tukio la kutisha, la kuumiza, au lisilo la kawaida. Tukio
hilo linaweza kumfanya mtu ahisi hofu, huzuni, au kukosa usalama hata baada
ya muda kupita.
Aina za Trauma (Types of Trauma)
• Trauma ya Kihisia au Kisaikolojia (Psychological/Emotional Trauma)
Hii hutokea baada ya matukio yanayoumiza kisaikolojia kama vile unyanyasaji,
ajali, vita, au kifo cha ghafla cha mtu wa karibu.
• Trauma ya Kimwili (Physical Trauma)
Hii ni majeraha ya mwili yanayosababishwa na ajali, mapigano, au
mashambulio ya kimwili.
• Trauma ya Maendeleo
(Developmental Trauma)
Hii hutokea utotoni kutokana na ukosefu wa upendo, malezi mabaya, au
unyanyasaji wa muda mrefu.
• Trauma ya Mkusanyiko
(Complex Trauma)
Hutokea pale mtu anapopitia matukio ya kiwewe mara kwa mara kwa muda
mrefu, mfano katika mazingira ya vita au manyanyaso ya kifamilia.
Sababu za Trauma
(Causes of Trauma)
• Ajali za barabarani au majanga ya asili
(kama mafuriko, tetemeko la ardhi).
• Vita au mashambulio ya kigaidi.
• Unyanyasaji wa kimwili, kingono, au wa kihisia.
• Kupoteza mtu wa karibu kwa ghafla.
• Magonjwa makubwa au upasuaji wa hatari.
• Kudhulumiwa au kuteswa kwa muda mrefu.
Madhara ya Trauma
(Effects of Trauma)
• Wasiwasi mkubwa, hofu, au msongo wa mawazo.
• Kukosa usingizi au ndoto mbaya.
• Kukosa hamu ya kula au kula kupita kiasi.
• Kujitenga na watu, au kutojiamini.
• Kumbukumbu za tukio kutokea tena
(flashbacks).
• Matatizo ya mwili kama maumivu ya kichwa, uchovu au shinikizo la damu.
Matibabu ya Trauma
(Treatment of Trauma)
• Tiba ya Kisaikolojia
(Psychotherapy / Counseling)
• CBT
(Cognitive Behavioral Therapy): Husaidia kubadilisha fikra hasi.
Mhubiri: Rev. Dr. Eliona Kimaro
Kwa maoni na ushauri:
Smu :+255655516053, +255754516053
YouTube : Rev. Dr. Eliona Kimaro TV
Barua Pepe: rev.kimaroe1@gmail.com
Информация по комментариям в разработке