KIJITONYAMA LUTHERAN CHURCH: IBADA YA EVENING GLORY: THE SCHOOL OF HEALING 02/ 07/ 2024

Описание к видео KIJITONYAMA LUTHERAN CHURCH: IBADA YA EVENING GLORY: THE SCHOOL OF HEALING 02/ 07/ 2024

KIJITONYAMA LUTHERAN CHURCH: IBADA YA EVENING GLORY: THE SCHOOL OF HEALING 02/ 07/ 2024

UJUMBE WA LEO: VITA YA KESHO YAKO
[SEHEMU YA PILI]
Hagai 2 : 9
Hesabu 13 : 31 - 33
Mithali 23 : 7
Hesabu 14 : 8 - 9
Yohana 5 : 5 - 9

Hagai 2 : 9

9 Utukufu wa mwisho wa nyumba hii utakuwa mkuu kuliko utukufu wake wa kwanza, asema Bwana wa majeshi; na katika mahali hapa nitawapa amani, asema Bwana wa majeshi.

Hesabu 13 : 31 - 33

31 Bali wale watu waliopanda pamoja naye wakasema, Hatuwezi kupanda tupigane na watu hawa; kwa maana wana nguvu kuliko sisi.

32 Wakawaletea wana wa Israeli habari mbaya ya ile nchi waliyoipeleleza, wakasema, Ile nchi tuliyopita kati yake ili kuipeleleza, ni nchi inayowala watu wanaoikaa; na watu wote tuliowaona ndani yake ni watu warefu mno.

33 Kisha, huko tuliwaona Wanefili, wana wa Anaki, waliotoka kwa hao Wanefili; tukajiona nafsi zetu kuwa kama mapanzi; nao ndivyo walivyotuona sisi.

Mithali 23 : 7

7 Maana aonavyo nafsini mwake, ndivyo alivyo. Akuambia, Haya, kula, kunywa; Lakini moyo wake hauwi pamoja nawe.

Hesabu 14 : 8 - 9

8 Ikiwa Bwana anatufurahia, atatuingiza katika nchi hii atupe iwe yetu, nayo ni nchi yenye wingi wa maziwa na asali.

9 Lakini msimwasi Bwana, wala msiwaogope wale wenyeji wa nchi, maana wao ni chakula kwetu; uvuli uliokuwa juu yao umeondolewa, naye Bwana yu pamoja nasi; msiwaogope.

Yohana 5 : 5 - 9

5 Na hapa palikuwa na mtu, ambaye amekuwa hawezi muda wa miaka thelathini na minane.

6 Yesu alipomwona huyu amelala, naye akijua ya kuwa amekuwa hali hiyo siku nyingi, alimwambia, Wataka kuwa mzima?

7 Yule mgonjwa akamjibu, Bwana, mimi sina mtu wa kunitia birikani, maji yanapotibuliwa; ila wakati ninapokuja mimi, mtu mwingine hushuka mbele yangu.

8 Yesu akamwambia, Simama,
jitwike godoro lako, uende.

9 Mara yule mtu akawa mzima, akajitwika godoro lake, akaenda. Nayo ilikuwa ni sabato siku hiyo.


AGENDA ZA MAOMBI
1. TOBA.
2. Shukrani kwa Miezi sita 2024.
3. Omba Neema ya Mungu.
4. Omba uwepo wa Bwana uende pamoja nawe.
5. Omba Mungu akuepushe na Majaribu yasiyobeba kitu kwa ajili yako.
6. Kuombea Akili


Mhubiri: Mwl. Eng. Googluck Mushi.

Kwa maombi na ushauri :
Mch. Kiongozi: Dr. Eliona Kimaro
Simu: +255 655 516 053, +255 754 516 053
Mch. Msaidizi: Anna Kuyonga
Simu: +255 713 553 443
YouTube: Kijitonyama Lutheran church
Barua Pepe: [email protected]

Комментарии

Информация по комментариям в разработке