KIJITONYAMA LUTHERAN CHURCH: IBADA YA EVENING GLORY (THE SCHOOL OF HEALING ) 18/ 09/ 2024

Описание к видео KIJITONYAMA LUTHERAN CHURCH: IBADA YA EVENING GLORY (THE SCHOOL OF HEALING ) 18/ 09/ 2024

KIJITONYAMA LUTHERAN CHURCH: IBADA YA EVENING GLORY (THE SCHOOL OF HEALING ) 18/ 09/ 2024

UJUMBE WA LEO: KUOMBA KINYUME NA VIZUIZI VINAVYOZUIA SAUTI YA MUNGU.

Wakolosai 3 : 16
Luka 1 : 28 - 31
Ayubu 33 : 14
Marko 4 : 13 - 15
Yohana 16 : 21 - 23
1 Nyakati 21 : 1
Mwanzo 3 : 1 - 5


Wakolosai 3 : 16

16 Neno la Kristo na likae kwa wingi ndani yenu katika hekima yote, mkifundishana na kuonyana kwa zaburi, na nyimbo, na tenzi za rohoni; huku mkimwimbia Mungu kwa neema mioyoni mwenu.

Luka 1 : 28 - 31

28 Akaingia nyumbani kwake akasema, Salamu, uliyepewa neema, Bwana yu pamoja nawe.

29 Naye akafadhaika sana kwa ajili ya maneno yake, akawaza moyoni, Salamu hii ni ya namna gani?

30 Malaika akamwambia, Usiogope, Mariamu, kwa maana umepata neema kwa Mungu.

31 Tazama, utachukua mimba na kuzaa mtoto mwanamume; na jina lake utamwita Yesu.

Ayubu 33 : 14

14 Kwa kuwa Mungu hunena mara moja, Naam, hata mara ya pili, ajapokuwa mtu hajali.

Marko 4 : 13 - 15

13 Akawaambia, Hamjui mfano huu? Basi mifano yote mtaitambuaje?

14 Mpanzi huyo hulipanda neno.

15 Hawa ndio walio kando ya njia lipandwapo neno; nao, wakiisha kusikia, mara huja Shetani, akaliondoa lile neno lililopandwa mioyoni mwao.

Yohana 16 : 21 - 23

21 Mwanamke azaapo, yuna huzuni kwa kuwa saa yake imefika; lakini akiisha kuzaa mwana, haikumbuki tena ile dhiki, kwa sababu ya furaha ya kuzaliwa mtu ulimwenguni.

22 Basi ninyi hivi sasa mna huzuni; lakini mimi nitawaona tena; na mioyo yenu itafurahi, na furaha yenu hakuna awaondoleaye.

23 Tena siku ile hamtaniuliza neno lo lote. Amin, amin, nawaambia, Mkimwomba Baba neno lo lote atawapa kwa jina langu.

1 Nyakati 21 : 1

1 Tena shetani akasimama juu ya Israeli, akamshawishi Daudi kuwahesabu Israeli.

Mwanzo 3 : 1 - 5

1 Basi nyoka alikuwa mwerevu kuliko wanyama wote wa mwitu aliowafanya Bwana Mungu. Akamwambia mwanamke, Ati! Hivi ndivyo alivyosema Mungu, Msile matunda ya miti yote ya bustani?

2 Mwanamke akamwambia nyoka, Matunda ya miti ya bustanini twaweza kula;

3 lakini matunda ya mti ulio katikati ya bustani Mungu amesema, Msiyale wala msiyaguse, msije mkafa.

4 Nyoka akamwambia mwanamke, Hakika hamtakufa,

5 kwa maana Mungu anajua ya kwamba siku mtakayokula matunda ya mti huo, mtafumbuliwa macho, nanyi mtakuwa kama Mungu, mkijua mema na mabaya.


Mhubiri: Mwl. Amani Mringo.

Kwa maombi na ushauri :
Mch. Kiongozi: Dr. Eliona Kimaro
Simu: +255 655 516 053, +255 754 516 053
Mch. Msaidizi: Anna Kuyonga
Simu: +255 713 553 443
YouTube: Kijitonyama Lutheran church
Barua Pepe: [email protected]

Комментарии

Информация по комментариям в разработке